Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima, akikabidhi zawadi maalum kwa Mwenyekiti Mwanawake Initiative Foundation (MIF) Mhe. Wanu Hafidh Ameir mara baada ya kuzindua Programu ya Uongozi kwa Wanawake Vijana, iliyoandaliwa na Taasisi za Care International Tanzania pamoja na Mwanawake Initiative Foundation (MIF). Tukio hili limefanyika Februari 11, 2025 jijini Dar Es Salaam
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima kuelekea Siku ya Wanawake Duniani mwaka 2025 ameonesha kwa Umma sare ya kitenge itakayotumika katika maadhimisho hayo nchini.
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mwananidi Ali Khamis akijibu hoja mbalimbali za Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii mara baada ya Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Bajeti ya Wizara kwa nusu ya mwaka wa fedha 2024/25 mbele ya Kamati Januari 23, 2025 Bungeni jijini Dodoma.
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Bajeti ya Wizara kwa nusu ya mwaka wa fedha 2024/25 mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii Januari 23, 2025 Bungeni jijini Dodoma
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Wakili Amon Mpanju akijibu hoja mbalimbali za Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii mara baada ya Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Bajeti ya Wizara kwa nusu ya mwaka wa fedha 2024/25 mbele ya Kamati Januari 23, 2025 Bungeni jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleoya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. akijibu hoja mbalimbali za Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii mara baada ya Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Bajeti ya Wizara kwa nusu ya mwaka wa fedha 2024/25 mbele ya Kamati hiyo Januari 23, 2025 Bungeni jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mwanaidi Ali Khamis akijibu hoja mbalimbali za Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii mara baada ya kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara Januari 22, 2025 jijini Dodoma.
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Amon Mpanju akijibu baadhi ya hoja kutoka kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii wakati Wizara ikiwasilisha taarifa yake ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara mbele ya Kamati hiyo Januari 22, 2025 jijini Dodoma.
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Programu ya Tanzania ya Kikazi chenye Usawa (GEF) pamoja na taarifa ya utekelezaji ya mfuko wa Maendeleo ya Wanawake (WDF) mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii Januari 22, 2025 jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe (ambaye alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum) (kushoto) akikabidhi rasmi Ofisi kwa Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu (kulia). Makabidhiano hayo yamefanyika leo Januari 20, 2025 katika Ofisi za Wizara jijini Dodoma baada ya mabadiliko yaliyofanywa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Januari 17, 2025.